MICHAEL MTANZANIA

ONESTEPMEDIATZ

AFRICAN LYON WATAKA KUJUA MDHAMINI WA LIGI KUU MSIMU UJAO, WASEMA HAWATAKI KUVULIWA JEZI UWANJANI

KLABU ya African Lyon ya Dar es Salaam imelitaka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kumtaja mdhamini wa msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, kufuatia kampuni ya Vodacom Tanzania kumaliza mkataba wake.



Hayo yamesemwa na mmiliki wa Lyon, Rahim Kangezi ‘Zamunda’ leo katika mahojiano maalum na Bin Zubeiry Sports – Online kutoka New York, Marekani.

Zamunda ambaye yupo Marekani kununua vifaa vya michezo kwa ajili ya timu yake amesema kwamba ikiwa sasa ni miezi miwili kabla ya msimu mpya wa Ligi Kuu kuanza, ni wakati mwafaka kwa TFF kumtaja mdhamini Mkuu wa Ligi Kuu.

Post a Comment

0 Comments