MICHAEL MTANZANIA

ONESTEPMEDIATZ

ZIFAHAMU SHEREHE ZINAZOITWA URS AMBAPO WATU HITAKATA MIGUU MIKONO NA KUTITOA MACHO YAO BILA GANZI

 Urs au Urus, wanaiita sherehe ya kifo wanayoifanya waislamu wale ambao ni wasufi, hufanya sherehe hizi kudhihirisha imani yao kali waliyonayo, katika sherehe hizi watu hukata miguu yao ha

dharani, hukata mikono yao na kuichoma moto, wengine hujichomoa hata macho live.


Haya yote hufanywa hadahari na bila ganzi yoyote, wengine hudiriki hata kujikata ndimi zao au hata kujichoma moto wenyewe wazima.

Wanasema kuwa hii yote inafanyika ili kuonyesha kuwa ni watu wenye imani kali kiasi gani, kuonyesha kuwa ni watu ambao huwaambii lolote linapokuja swala la kuhusu imani yao, imani yao ndio kila kitu kwao, hawa wanapatikana sana Asia hasa India.
Sherehe hizi hufanyika kila mwaka hasa katika mji wa Ajmer, Rajasthan India na wanasema mbali na kujionesha kua wana imani kiasi gani lakini pia hiyo ni kwaajili ya kuwakumbuka watakatifu wao katika dini hiyo waliokuwepo zaidi ya miaka 800 iliyopita.

Waislamu hawa wa Sufi wanasema kuwa wao ndiyo watetezi wa kweli wa asili ya Uislamu, wanafanya sherehe hizi kwa muda wa siku sita mfululizo kila mwaka, kwahivyo huko ni kawaida tuu kuona ndugu yako anatoka, halafu anarudi hana jicho au miguu. 

Post a Comment

0 Comments