MICHAEL MTANZANIA

ONESTEPMEDIATZ

Kocha Age Hareide amtema Nicklas Bendtner

Mshambuliaji Nicklas Bendtner ameondolewa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Denmark kitakachokwenda Urusi kushiriki fainali za kombe la dunia, zinazotarajiwa kuanza Juni 14.

Bendtner ameachwa kwenye kikosi cha mwisho cha wachezaji 23 wa nchi hiyo, kufuatia majeraha nyonga alioyapata akiwa katika klabu yake ya Rosenborg ya Norway juma moja kabla ya kujiunga na kikosi cha Denmark.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 30, alijaribu kufanya mazoezi na kikosi cha Denmark na kuonyesha maendeleo mazuri, pia alipata nafasi ya kucheza mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Sweden mjini Stockholm, juzi jumamosi.
Jana jumapili alifanyiwa mtihani wa mwisho wa upimaji wa afya, lakini hakuwaridhisha madaktari wa timu ya taifa ya Denmark na kupelekea kocha mkuu Age Hareide kumuacha sambamba na beki Andreas Bjelland.
“Hatuamini kama wataweza kuwa FIT kabla ya mchezo wetu dhidi ya Peru, tumewajaribu na imeonyesha hawapo katika hali nzuri ya kwenda kupambana katika fainali za kombe la dunia,” Alisema Hareide kupitia video iliyowekwa kwenye ukurasa wa Twitter wa chama cha soka nchini Denmark.

Post a Comment

0 Comments