MICHAEL MTANZANIA

ONESTEPMEDIATZ

Ahukumiwa Kuchapwa Kiboko Kimoja kwa Kumpa Mwanafunzi Mimba...!!!

 
 
Mahakama ya Wilaya ya Hai  Mkoani Kilimanjaro  imetoa hukumu ya kuchwapwa kiboko kimoja mwanafunzi wa kidato cha tatu shule ya sekondari Longoi wilaya hapo baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka na kumpa ujauzito mwanafunzi mwenzake wa shule hiyo
Akisoma hukumu hiyo  Hakimu  mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Agnes Muhina  mbele ya mwendesha mashtaka wa polisi , Valeria Banda, alisema kuwa anatoa hukumu hiyo baada ya kuridhishwa na ushaidi uliotolewa mahakamani  hapo usioacha shaka yoyote.
Kesi hiyo pia ilikuwa na mashahidi sita wa upande wa mashtaka akiwemo daktari wa hospitali ya Hai,dawati la jinsia na watoto na mama mzazi wa binti huyo, mwalimu na binti mwenyewe.
Ilidaiwa na mwendesha mashtaka wa polisi  kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo   Oktoba 10, 2015 saa 8.00  mchana katika kijiji cha Mkalama Wilayani humo ambapo alimbaka na kumpa ujauzito mwanafunzi mwenzake wa kidato cha tatu mwenye umri (16).

Post a Comment

0 Comments