MICHAEL MTANZANIA

ONESTEPMEDIATZ

MSANII SHILOLE AFICHUA SIRI ZAKE NA BARNABA

Jana malkia wa muziki Bongo, Shilole ameachia wimbo wake mpya uitwao Hatutoi Kiki. Kama zilivyo ngoma zake zilizopita, ngoma hii pia imeandikwa na Barnaba Classic.





Kwenye interview na kipindi cha Supermega Cha Kings Fm kinachoongozwa na Prince Ramalove, mrembo huyo ameweka wazi sababu za kupenda kumtumia Barnaba kwenye utunzi wa ngoma zake.

“Barnaba ananijulia sana katika uimbaji wangu, yaani akiandika ngoma,anauvaa uhusika wangu,” amesema Shilole.
Shilole amedai kuwa hiyo ndiyo sababu kubwa ya yeye kupenda kuandikiwa ngoma na mkali huyo wa High Table Sound.

Post a Comment

0 Comments